Tuesday, November 20, 2012

Mradi wa kusafirisha Gesi kutoka Mtwara - Dar es Salaam - Tanga - Mombasa

Huu ulikuwa ni Mchango wa Mh. Blandes, Gosbert Begumisa[CCM, Karagwe] kwenye Bunge la Bajeti tar 19 Agosti 2011 "Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba niruhusu nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya na kwa kuleta hotuba nzuri ya Bajeti." Aliongeza "Mheshimiwa Spika, mradi wa kutandaza bomba la gesi asilia kutoka Mtwara - Dar es Salaam - Tanga - Mombasa, katika Bajeti mbalimbali zilizopita za Wizara hii zilitenga fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu kwa nia ya kutandaza bomba la gesi kutoka Mtwara - Dar es Salaam - Tanga hadi Mombasa. Kule Mombasa gesi hii ilikuwa itumike kuzalisha umeme, inawezekana nia hii ilikuwa njema lakini kutokana na hali ya upungufu wa umeme hapa nchini na uhaba wa gesi nashauri tusipele ke gesi nje ya nchi wakati sisi wenyewe tunashida ya umeme. Tusubiri hadi pale tutakapopata umeme na gesi ya ziada ndio tufikirie kupeleka gesi nje ya nchi. Kwa sasa nia ya kupeleka gesi Mombasa isitishwe, ni vizuri katika kufanya majumuisho Mheshimiwa Waziri atupe msimamo wa Serikali katika suala hili". Hii ni taarifa ya Hansard ya Bunge na hakuna aliyewahi kusikika akikanusha mradi huu. Je, wanakusini wategemee kukombolewa na raslimali walizonazo kutoka kwenye lindi la umaskini? Toa maoni yako

No comments:

Post a Comment