Thursday, August 30, 2012

Kikao cha SEDO kwa Wanakusini Jpili tar 2nd Sept 2012 Mikocheni, Dar es Salaam

Habari za kazi? Natumai wote mu wazima.

Napenda kuwaarifu kikao cha maendeleo cha wadau wa kusini yaani Lindi na Mtwara kinatarajiwa kufanyika siku ya Jumapili, tarehe 2 Septemba 2012, saa 8 mchana nyumbani kwa Balozi General Makame Rashid pale Mikocheni jirani na flats za TPDC. Agenda za mkutano pamoja na zingine ni kujadili mipango ya maendeleo kusini, mradi wa ufundishaji sekondari za kusini na kutengeneza vitambulisho vya wanachama wa SEDO.

Tunaombwa tuhudhurie kwa wingi na kila mmoja amuarifu mdau wa kusini juu ya mkutano huu. Tafadhali pia, tunaombwa tuendelee kuuboresha mfuko wa taasisi yetu kwa manufaa ya ndugu zetu kusini na sisi pia kama wanachama.

Karibuni nyote tushiriki kwa DHATI kuijenga Lindi na Mtwara.

Geoffrey Idelphonce Mwambe
Chairman
South Eastern Development Organization (SEDO)
P.O.Box 14292 Dar es Salaam
Tel: +255 784 509891; +255 785 271644; +255 782503840
Blog: http://kusiniforum.blogspot.com

No comments:

Post a Comment