Tuesday, July 31, 2012

Vurugu Zaibuka Upya Malipo ya Korosho Tandahimba

Taarifa kutoka Wilaya ya Tandahimba zinasema kuwa vurugu zimeibuka upya wilayani humo kufuatia kutokamilishiwa malipo kwa wakulima wa korosho kufuatia kulipwa kwa awamu ya pili ya malipo hayo baada ya vurugu za awali.

SEDO inaiomba serikali kuwathamini wananchi wa kusini kwa kuhakikisha wanapata stahili ya jasho lao ili liwasaidie kupata mahitaji ya lazima kimaisha lakini pia kuwapeeleka watoto shule ili kuikwamua kusini kutoka kwenye umaskini. Mfumo huu wa stakabadhi ghalani unaonekana kulalamikiwa sana na wakulima wa korosho hasa wa mikoa ya kusini kuliko mahali kwingineko nchini.

Tunahitaji wanakusini kuungana na kuona kadhia hii inayotufanya kila uchao tunarudi nyuma kimaendeleo inaondoka kusini.

No comments:

Post a Comment