Sunday, October 09, 2011

Mbunge aanza kuchimba visima 60 jimboni


MBUNGE wa Kilwa Kaskazini  Muktadha Mangungu, ameanza kuchimba visima 60 vitakavyogharimu zaidi ya Sh720 milioni, katika  vijiji na shule za sekondari zenye tatizo  la maji.Hatua hiyo inalenga katika kuwawezesha wapiga kura wake, kuondokana na kero ya muda mrefu ya kukosa huduma za maji.  Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  uzinduzi wa uchimbaji  wa visima hivyo, uliofanyika katika Shule ya Sekondari Ilulu, Mangungu  alisema kwa muda mrefu,  wananchi wa jimbo hilo wamekuwa wakikabiliwa na tatizo  wa kukosa huduma za maji safi na salama.  Alisema tatizo hilo limesababisha wananchi na hasa wanawake kutoshiriki vyema katika shughuli za maendeleo.Alisema mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge alipokea maombi mengi  kuhusu mahitaji  maji na  Mangungu aliwaombwa wananchi katika jimbo hilo kumpa ushirikiano ili aweze kuwatumikia. Pia aliwataka kutumia vizuri  visima hivyo ili viweze kudumu  na kuwasaidia kwa kipindi kirefu.Kwa upande wake, mwalimu Sara Mlaponi wa Shule ya Sekondari  Ilulu, alisema msaada huyo umekuja  katika wakati mwafaka  na kwamba utaweza kuondoa tatizo maji katika jumuiya ya shule hiyo. Alisema tatizo la maji, lilikuwa linawalazimisha  wanafunzi kukatisha vipindi na kwenda kutafuta maji mtaani.

Chanzo - Mwananchi

No comments:

Post a Comment