Tuesday, September 13, 2011

Makufuli yavunjwa Machinga Complex

HALMASHAURI ya Manispaa ya Wilaya ya Ilala imeanza kuvunja  makufuli katika vizimba  vya Soko la Machinga Complex, ambavyo wamiliki wake hawajaanza kufanyia biashara.  Kuvunjwa kwa vizimba hivyo, kumekuja baada ya wafanyabiashara hao kukaidi amri ya manispaa hiyo, inayowataka waanze kuvitumia  ili kuondoa malalamiko kutoka kwa wafanyabishara wengine waliovikosa.   Agizo hilo la kuvunja makufuli,  lilitolewa wiki iliyopita na Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa soko hilo, Abubakar Rakesh, baada ya vizimba hivyo kukaa wa muda mrefu bila vikiwa havina bidhaa, jambo ambalo limeibua malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara waliokosa maeneo.   Kazi ya kuvunja makufuli hayo iliyoanza mwishoni mwa wiki iliyopita na kusimamiwa na  Meneja wa soko hilo, Teddy Kundi, chini ya ulinzi wa polisi.  Teddy alisema vizimba ammbavyo makufuli yake yamevunjwa ni vya wamiliki ambao hawapo. Hata hivyo aliwataka wamiliki wa vizimba hivyo ,kufuata bidhaa zao katika ofisi za Manispaa ya Ilala na  kulipia gharama za uvunjaji , kodi ya miezi ambayo vizimba havikufunguliwa na  gharama za kuhifadhi  bidhaa.  “Mizigo yao ipo , ndani ya siku thelathini wawe wamekuja kuchukua na kulipia gharama za uvunjaji, kodi wanazodaiwa na  gharama ya kuhifadhi mizigo yao,”alisema Teddy.  

Chanzo - Mwananchi

1 comment:

  1. Ni kweli maana Machinga Complex haikuwa ya wamachinga tunaowajua ila vigogo na ndugu zao. Tuwape nafasi vijana na tuwaboreshee mazingira yao ya biashara kama tunavyoboresha ya wawekezaji kutoka nje ya nchi

    ReplyDelete