Tuesday, September 27, 2011

Waliosoma Kusini waaswa kuchangia elimu

MBUNGE wa Jimbo la Lindi Mjini, Salum Baruany - pichani amewashauri watu waliowahi

kusoma katika mikoa ya Kusini mwa Tanzania kushirikiana katika kufanikisha tamasha la

kuchangia maendeleo ya elimu kwa ajili ya mikoa hiyo. Baruany aliyasema hayo juzi katika

kikao cha maandalizi ya tamasha la kuchangia maendeleo ya elimu kwa mikoa ya Lindi,

Mtwara na Ruvuma kilichofanyika Ukumbi wa Imasco, Temeke jijini Dar es Salaam. Akiwa

mmoja wa waalikwa wa vikao hivyo vya kila wiki, Baruany alielezea kukunwa kwake na

ubunifu wa baadhi ya wanafunzi walioamua kuwahamasisha wenzao kukumbuka walikotoka

kielimu, kwa lengo la kuwainua wengine. “Nawapongeza sana. Ni wachache wanaoweza

kukumbuka walikotoka, hasa kielimu. Hapa mmelenga, mikoa ya kusini iko nyuma kielimu,

naamini wa kusaidia kupandisha hadhi ni ninyi wenyewe mliosoma kule na wadau wengine

wanaoguswa na suala hili. “Msikate tamaa, mtafanikiwa. Cha msingi ni kuwashirikisha na

kuwashawishi wengine waliosoma ana kuwa karibu na mazingira ya kielimu ya mikoa hii.

Nchi hujengwa na wananchi wenye moyo, nanyi kwa kuguswa kwenu, naamini elimu ya

kusini itainuka kwa sababu ni vigumu mtu mmoja mmoja kuchangia na bado maendeleo ya

kweli yakaonekana, bali kupitia mshikamano kama wenu,” alisema mbunge huyo. Naye

Mratibu wa tamasha hilo, Asanterabbi Mtaki, licha ya kumshukuru mbunge huyo kwa nasaha

zake, aliwataka wadau wa elimu nchini kuungana na waliosoma mikoa ya kusini ili k

ufanikisha azma ya kuiinua kusini kielimu. “Tangu awali tumeelezea hali ya elimu ya mikoa

ya Kusini, kwa kweli si nzuri na inahitajika nguvu ya ziada, ndiyo maana tumeungana

kuhakikisha tunafanikisha kitu kwa ajili ya shule za kusini na wanafunzi wake, hasa yatima,

walemavu na wasiojiweza ili wapate haki ya kupata elimu bora,” alisema Mtaki. Alisisitiza

kuwa, kasi ya maandalizi ya tamasha hilo inaridhisha na kuongeza kuwa, nafasi ya waliosoma

kusini kuchangia mawazo bado ipo, hasa kupitia vikao vya kila mwisho wa wiki

vinavyofanyika ukumbi wa Imasco.

No comments:

Post a Comment